1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,
2 kama umetegwa na ulichosema,
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,
4 Usiruhusu usingizi machoni pako,
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji,
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa;
7 Kwa maana yeye hana msimamizi,
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi
9 Ewe mvivu, utalala hata lini?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi,
12 Mtu mbaya sana na mlaghai,
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake,
14 ambaye hupanga ubaya
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula;
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana,
17 macho ya kiburi,
18 moyo uwazao mipango miovu,
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo,
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako,
21 Yafunge katika moyo wako daima,
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza;
23 Kwa maana amri hizi ni taa,
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka,
25 Moyo wako usitamani uzuri wake
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini,
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine;
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa,
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;
33 Mapigo na aibu ni fungu lake
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,
35 Hatakubali fidia yoyote;