1 Nilimlilia Mungu ili anisaidie,
2 Nilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana,
3 Ee Mungu, nilikukumbuka wewe, nikalia kwa huzuni;
4 Ulizuia macho yangu kufumba;
5 Nilitafakari juu ya siku zilizopita,
6 nilikumbuka nilivyoimba nyimbo usiku.
7 “Je, Bwana atakataa milele?
8 Je, upendo wake usio na mwisho umetoweka milele?
9 Je, Mungu amesahau kuwa na huruma?
10 Ndipo nikawaza, “Huu ndio udhaifu wangu:
11 Nitayakumbuka matendo ya Bwana;
12 Nitazitafakari kazi zako zote
13 Ee Mungu, njia zako ni takatifu.
14 Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza,
15 Kwa mkono wako wenye nguvu umewakomboa watu wako,
16 Maji yalikuona, Ee Mungu,
17 Mawingu yalimwaga maji,
18 Ngurumo yako ilisikika katika upepo wa kisulisuli,
19 Njia yako ilipita baharini,
20 Uliongoza watu wako kama kundi