1 Ee Mungu, uniokoe na adui zangu,
2 Uniponye na watu watendao mabaya,
3 Tazama wanavyonivizia!
4 Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia.
5 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli!
6 Hurudi wakati wa jioni,
7 Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao,
8 Lakini wewe, Bwana, uwacheke;
9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe,
10 Mungu wangu unipendaye.
11 Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu,
12 Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao,
13 wateketeze katika ghadhabu,
14 Hurudi jioni,
15 Wanatangatanga wakitafuta chakula,
16 Lakini mimi nitaziimba nguvu zako,
17 Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa.