1 Mpeni Bwana, enyi mashujaa,
2 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
3 Sauti ya Bwana iko juu ya maji;
4 Sauti ya Bwana ina nguvu;
5 Sauti ya Bwana huvunja mierezi;
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,
7 Sauti ya Bwana hupiga kwa miali
8 Sauti ya Bwana hutikisa jangwa;
9 Sauti ya Bwana huzalisha ayala,
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;
11 Bwana huwapa watu wake nguvu;