1 Nakupenda wewe, Ee Bwana,
2 Bwana ni mwamba wangu,
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa,
4 Kamba za mauti zilinizunguka,
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka,
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana,
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika,
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake,
9 Akazipasua mbingu akashuka chini,
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka,
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika,
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni,
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui,
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa,
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika;
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi,
18 Walinikabili siku ya msiba wangu,
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele,
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu;
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana;
22 Sheria zake zote zi mbele yangu,
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake,
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu;
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu,
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu,
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu,
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka;
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi,
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu,
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita;
35 Hunipa ngao yako ya ushindi,
36 Huyapanua mapito yangu,
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata,
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena;
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo;
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu;
44 Mara wanisikiapo hunitii,
45 Wote wanalegea,
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu!
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi,
48 aniokoaye na adui zangu.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana;
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu,