1 Msifuni Bwana.
2 Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,
3 Nyumbani mwake kuna mali na utajiri,
4 Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu,
5 Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba,
6 Hakika hatatikisika kamwe,
7 Hataogopa habari mbaya,
8 Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu,
9 Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini;
10 Mtu mwovu ataona na kuchukizwa,