1 Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu;
2 Ninawapa mafundisho ya maana,
3 Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu,
4 baba alinifundisha akisema,
5 Pata hekima, pata ufahamu;
6 Usimwache hekima naye atakuweka salama;
7 Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima.
8 Mstahi, naye atakukweza;
9 Atakuvika shada la neema kichwani mwako
10 Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia,
11 Ninakuongoza katika njia ya hekima
12 Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa;
13 Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;
14 Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu
15 Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo;
16 Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu;
17 Wanakula mkate wa uovu,
18 Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko,
19 Lakini njia ya waovu ni kama giza nene;
20 Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia;
21 Usiruhusu yaondoke machoni pako,
22 kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata
23 Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo,
24 Epusha kinywa chako na ukaidi;
25 Macho yako na yatazame mbele,
26 Sawazisha mapito ya miguu yako
27 Usigeuke kulia wala kushoto;