1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa,
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana,
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu,
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe,
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki,
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu,
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka,
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake,
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi,
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake,
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya,
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi,
14 Kutokana na tunda la midomo yake
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja,
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika,
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga,
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele,
20 Upo udanganyifu katika mioyo
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki,
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo,
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe,
24 Mikono yenye bidii itatawala,
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu,
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki,
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake,
28 Katika njia ya haki kuna uzima;