Números 33

SWHONEN vs NAA

Sair da comparação
NAA Nova Almeida Atualizada 2017
1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
1 São estas as caminhadas dos filhos de Israel que saíram da terra do Egito, segundo os seus exércitos, sob as ordens de Moisés e Arão.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
2 Moisés escreveu os lugares de que saíram, caminhada após caminhada, conforme o mandado do Senhor . E são estas as suas caminhadas, segundo os lugares de que saíram:
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
3 eles partiram de Ramessés no décimo quinto dia do primeiro mês. No dia seguinte ao da Páscoa, os filhos de Israel saíram, corajosamente, aos olhos de todos os egípcios,
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
4 enquanto estes sepultavam todos os seus primogênitos, a quem o Senhor havia matado entre eles; também contra os deuses o Senhor executou juízos.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
5 Os filhos de Israel partiram de Ramessés e acamparam em Sucote.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
6 Partiram de Sucote e acamparam em Etã, que está no fim do deserto.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
7 Partiram de Etã e voltaram a Pi-Hairote, que está diante de Baal-Zefom, e acamparam diante de Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
8 Partiram de Pi-Hairote, passaram pelo meio do mar em direção ao deserto e, depois de terem caminhado três dias no deserto de Etã, acamparam em Mara.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
9 Partiram de Mara e chegaram a Elim. Em Elim, havia doze fontes de água e setenta palmeiras; e acamparam ali.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
10 Partiram de Elim e acamparam junto ao mar Vermelho.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
11 Partiram do mar Vermelho e acamparam no deserto de Sim.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
12 Partiram do deserto de Sim e acamparam em Dofca.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
13 Partiram de Dofca e acamparam em Alus.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
14 Partiram de Alus e acamparam em Refidim, porém ali não havia água para o povo beber.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
15 Partiram de Refidim e acamparam no deserto do Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
16 Partiram do deserto do Sinai e acamparam em Quibrote-Hataavá.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
17 Partiram de Quibrote-Hataavá e acamparam em Hazerote.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
18 Partiram de Hazerote e acamparam em Ritma.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
19 Partiram de Ritma e acamparam em Rimom-Perez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
20 Partiram de Rimom-Perez e acamparam em Libna.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
21 Partiram de Libna e acamparam em Rissa.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
22 Partiram de Rissa e acamparam em Queelata.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
23 Partiram de Queelata e acamparam no monte Sefer.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
24 Partiram do monte Sefer e acamparam em Harada.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
25 Partiram de Harada e acamparam em Maquelote.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
26 Partiram de Maquelote e acamparam em Taate.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
27 Partiram de Taate e acamparam em Tera.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
28 Partiram de Tera e acamparam em Mitca.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
29 Partiram de Mitca e acamparam em Hasmona.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
30 Partiram de Hasmona e acamparam em Moserote.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
31 Partiram de Moserote e acamparam em Benê-Jaacã.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
32 Partiram de Benê-Jaacã e acamparam em Hor-Hagidgade.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
33 Partiram de Hor-Hagidgade e acamparam em Jotbatá.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
34 Partiram de Jotbatá e acamparam em Abrona.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
35 Partiram de Abrona e acamparam em Eziom-Geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
36 Partiram de Eziom-Geber e acamparam no deserto de Zim, que é Cades.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
37 Partiram de Cades e acamparam no monte Hor, na fronteira da terra de Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
38 Então Arão, o sacerdote, subiu o monte Hor, segundo o mandado do Senhor ; e morreu ali, no primeiro dia do quinto mês do quadragésimo ano depois da saída dos filhos de Israel da terra do Egito.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
39 Arão tinha cento e vinte e três anos de idade quando morreu no monte Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
40 Então o rei cananeu de Arade, que habitava o Sul da terra de Canaã, soube que os filhos de Israel estavam chegando.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
41 Eles partiram do monte Hor e acamparam em Zalmona.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
42 Partiram de Zalmona e acamparam em Punom.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
43 Partiram de Punom e acamparam em Obote.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
44 Partiram de Obote e acamparam em Ijé-Abarim, na fronteira de Moabe.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
45 Partiram de Ijé-Abarim e acamparam em Dibom-Gade.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
46 Partiram de Dibom-Gade e acamparam em Almom-Diblataim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
47 Partiram de Almom-Diblataim e acamparam nos montes de Abarim, diante de Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
48 Partiram dos montes de Abarim e acamparam nas campinas de Moabe, junto ao Jordão, na altura de Jericó.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
49 E acamparam junto ao Jordão, desde Bete-Jesimote até Abel-Sitim, nas campinas de Moabe.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
50 Nas campinas de Moabe, junto ao Jordão, na altura de Jericó, o Senhor disse a Moisés:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
51 — Fale com os filhos de Israel e diga-lhes: Quando vocês tiverem passado o Jordão para entrar na terra de Canaã,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
52 devem expulsar da frente de vocês todos os moradores da terra, destruir todas as pedras com figura e todas as imagens fundidas. Devem também derrubar todos os santuários nos lugares altos.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
53 Tomem posse da terra e morem nela, porque eu lhes dei esta terra, para que vocês tomem posse dela.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
54 Vocês herdarão a terra por sorteio, segundo as suas famílias. À tribo mais numerosa deem uma herança maior; à tribo pequena deem uma herança menor. Onde lhe cair a sorte, esse lugar lhe pertencerá; vocês herdarão segundo as tribos de seus pais.
55 “ ‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
55 Porém, se não expulsarem os moradores da terra, então os que vocês deixarem ficar serão para vocês como espinhos nos olhos e como aguilhões nas costas e eles os perturbarão na terra em que vocês irão morar.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’ ”
56 E farei com vocês o que pensei fazer com eles.

Ler em outra tradução

Comparar com outra