1 “Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa?
2 Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo?
3 Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao;
4 Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani;
5 “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru?
6 Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake,
7 Huzicheka ghasia za mji,
8 Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho
9 “Je, nyati atakubali kukutumikia?
10 Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba?
11 Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi?
12 Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani
13 “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha,
14 Huyataga mayai yake juu ya ardhi,
15 bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda,
16 Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake;
17 kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima,
18 Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia,
19 “Je, wewe humpa farasi nguvu
20 Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige,
21 Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake,
22 Huicheka hofu, haogopi chochote,
23 Podo hutoa sauti kando yake,
24 Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi,
25 Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’
26 “Je, mwewe huruka kwa hekima yako
27 Je, tai hupaa juu kwa amri yako
28 Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku;
29 Kutoka huko hutafuta chakula chake;
30 Makinda yake hujilisha damu,