1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza
3 Jikaze kama mwanaume;
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake,
10 nilipoamuru mipaka yake,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi;
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke,
13 yapate kushika miisho ya dunia,
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri;
15 Waovu huzuiliwa nuru yao,
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia?
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu,
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa,
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa,
28 Je, mvua ina baba?
29 Barafu inatoka tumbo la nani?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe,
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake,
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni,
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu?
38 wakati mavumbi yawapo magumu,
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao,
41 Ni nani ampaye kunguru chakula