1 “Kuna machimbo ya fedha,
2 Chuma hupatikana ardhini,
3 Mwanadamu hukomesha giza;
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu,
5 Ardhi, ambako chakula hutoka,
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake,
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika,
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga,
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana,
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba;
11 Hutafuta vyanzo vya mito
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake;
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’;
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote,
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri,
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo,
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa;
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo,
20 “Ni wapi basi hekima itokako?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai,
22 Uharibifu na Mauti husema,
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia
25 Alipofanyiza nguvu za upepo
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake,
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu,