1 Ndipo Ayubu akajibu:
2 “Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini,
3 Mara kumi hizi mmenishutumu;
4 Kama ni kweli nimepotoka,
5 Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu,
6 basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya,
7 “Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu;
8 Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita;
9 Amenivua heshima yangu,
10 Amenibomoa kila upande hadi nimeisha;
11 Hasira yake imewaka juu yangu;
12 Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu;
13 “Amewatenga ndugu zangu mbali nami;
14 Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali;
15 Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni;
16 Namwita mtumishi wangu, wala haitiki,
17 Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu;
18 Hata watoto wadogo hunidhihaki;
19 Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa;
20 Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu;
21 “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma,
22 Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo?
23 “Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu,
24 kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma,
25 Ninajua kwamba Mkombozi wangu yu hai,
26 Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa,
27 mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe:
28 “Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda,
29 ninyi wenyewe uogopeni upanga,