1 Bildadi Mshuhi akajibu:
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya?
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama,
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande
5 “Taa ya mwovu imezimwa,
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza;
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa;
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu,
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino;
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake;
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande,
12 Janga linamwonea shauku;
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake;
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake,
15 Moto utakaa katika hema lake;
16 Mizizi yake chini itakauka
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia,
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani,
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake,
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata;
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu;