1 Kisha Elifazi Mtemani akajibu:
2 “Je, mtu mwenye hekima hujibu kwa mawazo matupu,
3 Je, aweza kubishana juu ya maneno yasiyofaa,
4 Lakini unadhoofisha hata uchaji wa Mungu
5 Dhambi yako inasukuma kinywa chako,
6 Kinywa chako mwenyewe kinakuhukumu, wala si changu;
7 “Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa?
8 Je, wewe husikiliza mashauri ya siri ya Mungu?
9 Wewe unajua kitu gani tusichokijua sisi?
10 Wale wenye mvi na wazee wako upande wetu,
11 Je, faraja za Mungu hazikutoshi,
12 Kwa nini moyo wako unakudanganya,
13 ili kwamba upate kutoa hasira yako dhidi ya Mungu,
14 “Mwanadamu ni kitu gani, hata aweze kuwa safi,
15 Kama Mungu hawaamini watakatifu wake,
16 sembuse mwanadamu ambaye ni mwovu na mpotovu,
17 “Nisikilize mimi nami nitakueleza,
18 ambayo watu wenye hekima wameyanena,
19 (wakati ambao wao peke yao ndio walipewa nchi,
20 Mtu mwovu siku zake zote hupata mateso,
21 Sauti za kutisha hujaa masikioni mwake;
22 Hukata tamaa kuokoka gizani;
23 Hutangatanga, akitafuta chakula;
24 Taabu na maumivu makuu vinamtia hofu;
25 kwa sababu amemkunjia Mungu ngumi yake
26 kwa kiburi akishambulia dhidi ya Mungu
27 “Ingawa uso wake umefunikwa na mafuta kwa unene
28 ataishi katika miji ya magofu,
29 Hatatajirika tena, nao utajiri wake hautadumu,
30 Hatatoka gizani;
31 Asijidanganye mwenyewe kutumainia ubatili,
32 Atakuwa amelipwa kikamilifu kabla ya wakati wake,
33 Atafanana na mzabibu uliopukutishwa matunda yake kabla hayajaiva,
34 Kwa kuwa jamii ya wasiomcha Mungu watakuwa tasa,
35 Hutunga mimba ya madhara na kuzaa uovu;