1 “Nayachukia sana haya maisha yangu;
2 Nitamwambia Mungu: Usinihukumu,
3 Je, inakupendeza wewe kunionea,
4 Je, wewe una macho ya kimwili?
5 Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu,
6 ili kwamba utafute makosa yangu
7 ingawa wajua kuwa mimi sina hatia,
8 “Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya.
9 Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi.
10 Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa,
11 ukanivika ngozi na nyama,
12 Umenipa uhai na kunitendea wema,
13 “Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako,
14 Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona,
15 Kama nina hatia, ole wangu!
16 Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba,
17 Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu
18 “Kwa nini basi ulinitoa tumboni?
19 Laiti nisingekuwako kamwe,
20 Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha?
21 kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena,
22 nchi ya giza kuu sana,