1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema:
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme,
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu,
9 Sio wazee peke yao walio na hekima,
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi;
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea,
12 niliwasikiliza kwa makini.
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima;
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu,
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema;
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya,
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema;
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno,
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai,
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia;
21 Sitampendelea mtu yeyote,
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza,