1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki,
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu,
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa,
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi,
5 Walifukuzwa mbali na watu wao,
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka,
7 Kwenye vichaka walilia kama punda,
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya,
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo;
10 Wananichukia sana na kujitenga nami,
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa,
12 Kuume kwangu kundi linashambulia;
13 Huizuia njia yangu,
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana;
15 Vitisho vimenifunika;
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho;
17 Usiku mifupa yangu inachoma;
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo;
19 Yeye amenitupa kwenye matope,
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu;
21 Wewe unanigeukia bila huruma;
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo;
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni,
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji,
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia;
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii;
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua;
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha,
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika;
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo,