1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 Wana wa Yafethi walikuwa:
3 Wana wa Gomeri walikuwa:
4 Wana wa Yavani walikuwa:
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 Wana wa Hamu walikuwa:
7 Wana wa Kushi walikuwa:
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 Misraimu alikuwa baba wa:
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Kanaani alikuwa baba wa:
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 Wana wa Shemu walikuwa:
23 Wana wa Aramu walikuwa:
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela,
25 Eberi akapata wana wawili:
26 Yoktani alikuwa baba wa:
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.