Eclesiastes 3

SWHONEN

1 Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo,

2 wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa,

3 wakati wa kuua na wakati wa kuponya,

4 wakati wa kulia na wakati wa kucheka,

5 wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe,

6 wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza,

7 wakati wa kurarua na wakati wa kushona,

8 wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia,

9 Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake?

10 Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu.

11 Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho.

12 Ninajua kwamba hakuna kitu bora kwa wanadamu kuliko kuwa na furaha na kutenda mema wakati wanapoishi.

13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.

14 Ninajua kwamba kila kitu anachokifanya Mungu kitadumu milele, hakuna kinachoweza kuongezwa au kupunguzwa. Mungu hufanya hivyo ili watu wamche yeye.

15 Chochote kilichopo kilishakuwepo,

16 Pia nikaona kitu kingine tena chini ya jua:

17 Nikafikiri moyoni mwangu,

18 Pia nikafikiri, “Kuhusu wanadamu, Mungu huwajaribu ili wajione kwamba wao ni kama wanyama.

19 Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili.

20 Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.

21 Ni nani ajuaye kama roho ya mtu huenda juu na roho ya mnyama hushuka chini ardhini?”

22 Kwa hiyo nikaona kwamba hakuna kitu kilicho bora zaidi kwa mwanadamu kuliko kuifurahia kazi yake, kwa sababu hilo ndilo fungu lake. Kwa maana ni nani awezaye kumrudisha ili aje kuona kile kitakachotendeka baada yake?

Ler em outra tradução

Comparar lado a lado