1 Crônicas 6

SWHONEN

1 Wana wa Lawi walikuwa:

2 Wana wa Kohathi walikuwa:

3 Amramu alikuwa na wana:

4 Eleazari akamzaa Finehasi,

5 Abishua akamzaa Buki,

6 Uzi akamzaa Zerahia,

7 Merayothi akamzaa Amaria,

8 Ahitubu akamzaa Sadoki,

9 Ahimaasi akamzaa Azaria,

10 Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),

11 Azaria akamzaa Amaria,

12 Ahitubu akamzaa Sadoki,

13 Shalumu akamzaa Hilkia,

14 Azaria akamzaa Seraya,

15 Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.

16 Wana wa Lawi walikuwa:

17 Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni:

18 Wana wa Kohathi walikuwa:

19 Wana wa Merari walikuwa:

20 Wazao wa Gershoni:

21 Zima akamzaa Yoa,

22 Wazao wa Kohathi:

23 Asiri akamzaa Elikana,

24 Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli,

25 Wazao wa Elikana walikuwa:

26 Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai,

27 Nahathi akamzaa Eliabu,

28 Wana wa Samweli walikuwa:

29 Wafuatao ndio wazao wa Merari:

30 Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia,

31 Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.

32 Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.

33 Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao:

34 mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu,

35 mwana wa Sufu, mwana wa Elikana,

36 mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli,

37 mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri,

38 mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi,

39 na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume:

40 mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya,

41 mwana wa Ethni,

42 mwana wa Ethani, mwana wa Zima,

43 mwana wa Yahathi,

44 Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto:

45 mwana wa Hashabia,

46 mwana wa Amsi, mwana wa Bani,

47 mwana wa Mahli,

48 Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.

49 Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.

50 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni:

51 Abishua akamzaa Buki,

52 Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria,

53 Ahitubu akamzaa Sadoki,

54 Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):

55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.

56 Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.

57 Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,

58 Hileni, Debiri,

59 Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.

60 Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho.

61 Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.

62 Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.

63 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.

64 Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.

65 Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.

66 Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.

67 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,

68 Yokmeamu, Beth-Horoni,

69 Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.

70 Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.

71 Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho:

72 Kutoka kabila la Isakari

73 Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.

74 Kutoka kabila la Asheri

75 Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.

76 Kutoka kabila la Naftali

77 Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo:

78 Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko

79 Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.

80 Na kutoka kabila la Gadi

81 Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.

Ler em outra tradução

Comparar lado a lado