Números 26

SWHONEN

1 Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,

2 “Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”

3 Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,

4 “Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.”

5 Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa:

6 kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni;

7 Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.

8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,

9 nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.

10 Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.

11 Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.

12 Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa:

13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera;

14 Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.

15 Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa:

16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni;

17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi;

18 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.

19 Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.

20 Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa:

21 Wazao wa Peresi walikuwa:

22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.

23 Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa:

24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu;

25 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.

26 Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa:

27 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.

28 Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:

29 Wazao wa Manase:

30 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi:

31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli;

32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida;

33 (Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)

34 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.

35 Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao:

36 Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela:

37 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500.

38 Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa:

39 kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu;

40 Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa:

41 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.

42 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao:

43 Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.

44 Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa:

45 kutoka kwa wazao wa Beria:

46 (Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)

47 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.

48 Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa:

49 kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri;

50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.

51 Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.

52 Bwana akamwambia Mose,

53 “Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.

54 Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.

55 Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.

56 Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”

57 Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao:

58 Hizi pia zilikuwa koo za Walawi:

59 jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.

60 Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.

61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)

62 Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.

63 Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.

64 Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.

65 Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.

Ler em outra tradução

Comparar lado a lado