1 Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu:
2 Abrahamu akamzaa Isaki,
3 Yuda akawazaa Peresi na Zera, ambao mama yao alikuwa Tamari,
4 Aramu akamzaa Aminadabu,
5 Salmoni akamzaa Boazi, na mama yake Boazi alikuwa Rahabu,
6 Yese akamzaa Daudi ambaye alikuwa mfalme.
7 Solomoni akamzaa Rehoboamu,
8 Asa akamzaa Yehoshafati,
9 Uzia akamzaa Yothamu,
10 Hezekia akamzaa Manase,
11 wakati wa uhamisho wa Babeli, Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake.
12 Baada ya uhamisho wa Babeli:
13 Zerubabeli akamzaa Abiudi,
14 Azori akamzaa Sadoki,
15 Eliudi akamzaa Eleazari,
16 naye Yakobo akamzaa Yosefu ambaye alikuwa mumewe Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
17 Hivyo, kulikuwepo na jumla ya vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi hadi wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli, na vizazi kumi na vinne tangu wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli hadi Kristo.
18 Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria alionekana kuwa na mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
19 Kwa kuwa Yosefu, mwanaume aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani, aliazimu kumwacha kwa siri.
20 Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na kusema, “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
21 Naye atamzaa mwana, nawe utamwita Jina lake Yesu, kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka dhambi zao.”
22 Haya yote yalitukia ili litimie lile Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii, akisema:
23 “Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli”: maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
24 Yosefu alipoamka kutoka usingizini, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake.
25 Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria alipojifungua mwanawe kifungua mimba akamwita Jina lake Yesu.