1 Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.
2 “Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo,
3 “Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza,
4 Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena,
5 “Simeoni na Lawi ni wana ndugu:
6 Mimi na nisiingie katika baraza lao,
7 Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno,
8 “Yuda, ndugu zako watakusifu;
9 Ee Yuda, wewe ni mwana simba;
10 Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda,
11 Atamfunga punda wake katika mzabibu,
12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai,
13 “Zabuloni ataishi pwani ya bahari
14 “Isakari ni punda mwenye nguvu
15 Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika
16 “Dani atahukumu watu wake kwa haki
17 Dani atakuwa nyoka kando ya barabara,
18 “Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.
19 “Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji,
20 “Chakula cha Asheri kitakuwa kinono,
21 “Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru
22 “Yosefu ni mzabibu uzaao,
23 Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia,
24 Lakini upinde wake ulibaki imara,
25 kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia,
26 Baraka za baba yako ni kubwa
27 “Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu;
28 Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.
29 Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti,
30 pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba.
31 Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea.
32 Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”
33 Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.