Ezequiel 30

SWHONEN

1 Neno la Bwana likanijia kusema:

2 “Mwanadamu, toa unabii na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

3 Kwa kuwa siku ile imekaribia,

4 Upanga utakuja dhidi ya Misri,

5 Kushi na Putu, Ludi na Arabia yote, Libya na watu wa nchi ya Agano watauawa kwa upanga pamoja na Misri.

6 “ ‘Hili ndilo Bwana asemalo:

7 “ ‘Hizo nchi zitakua ukiwa

8 Ndipo watakapojua kwamba mimi ndimi Bwana,

9 “ ‘Siku hiyo wajumbe watatoka kwangu kwa merikebu, ili kuwatia hofu Ethiopia, wakiwa katika hali yao ya kuridhika. Maumivu makali yatawapata siku ya maangamizi ya Misri, kwa kuwa hakika itakuja.

10 “ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

11 Yeye na jeshi lake, taifa lililo katili kuliko mataifa yote,

12 Nitakausha vijito vya Naili

13 “ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

14 Nitaifanya Pathrosi kuwa ukiwa

15 Nitaimwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu,

16 Nitaitia moto nchi ya Misri;

17 Wanaume vijana wa Oni na wa Pi-Besethi

18 Huko Tahpanhesi mchana utatiwa giza

19 Kwa hiyo nitaipiga Misri kwa adhabu,

20 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa kwanza, siku ya saba, neno la Bwana likanijia kusema:

21 “Mwanadamu, nimevunja mkono wa Farao mfalme wa Misri. Haukufungwa ili upone au kuwekewa kipande cha ubao ili upate nguvu za kuweza kuchukua upanga.

22 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na Farao mfalme wa Misri. Nitavunja mikono yake yote miwili, ule mkono ulio mzima pia na ule uliovunjika na kuufanya upanga uanguke toka mkononi mwake.

23 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.

24 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli na kuutia upanga wangu mkononi mwake, lakini nitavunja mikono ya Farao, naye atalia kwa huzuni mbele yake kama mtu aliyetiwa jeraha la kumfisha.

25 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli, lakini mikono ya Farao italegea. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye ataunyoosha dhidi ya Misri.

26 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi mbalimbali. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”

Ler em outra tradução

Comparar lado a lado