1 Crônicas 24

SWHONEN

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni:

2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.

3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.

4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.

5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.

6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.

7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu,

8 ya tatu Harimu,

9 ya tano Malkiya,

10 ya saba Hakosi,

11 ya tisa Yeshua,

12 ya kumi na moja Eliashibu,

13 ya kumi na tatu Hupa,

14 ya kumi na tano Bilga,

15 ya kumi na saba Heziri,

16 ya kumi na tisa Pethahia,

17 ya ishirini na moja Yakini,

18 ya ishirini na tatu Delaya,

19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.

20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki:

21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe:

22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi,

23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.

24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika;

25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia;

26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi.

27 Wana wa Merari:

28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.

29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi:

30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi.

31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.

Ler em outra tradução

Comparar lado a lado